Rais Uhuru awakemea vikali wanasiasa wa NASA, atoa ombi maalum kwa Wakenya

July 2024 · 2 minute read

- Rais Uhuru Kenyatta ametetea hatamu yake ya kwanza kama rais kwa kusuta wapinzani wake- muungano wa NASA

- Akizungumza Nandi hills alipokuwa akifanya kampeni mnamo Jumatatu Juni 12, Uhuru alisema kwamba Raila na timu yake hawajawahi kufanyia Kenya lolote

- Uhuru aliwahimiza wafuasi wa Jubilee kuwauliza Raila na timu yake kutangaza walichofanikisha walipokuwa uongozini

Rais Uhuru Kenyatta alipokuwa akifanya kampeni Nandi Hills alichukua fursa hiyo kukashifu wapinzani wake, muungano wa NASA.

Habari Nyingine: Zari afichua KILICHOMUUA mume wake wa zamani, sio sumu

NASA inayoshikilia dhana kuwa Jubilee imekosa kutimiza ahadi ilizotoa kwa Wakenya 2013, imekuwa kila mara ikiwaeleza Wakenya kuwarusha nje Uhuruto .

Kutokana na haya, Uhuru aliwahimiza wakazi wa Nandi Hills kumwagiza Raila na timu yake kuwaeleza Wakenya walichofanikisha walipokuwa kwenye nyadhifa za serikali.

"Wapinzani wetu wanaposema hatujafanya lolote waambie wawaonyeshe walichiowafanyia Wakenya kwa miaka waliokuwa katika nyadhifa za uongozi,” Uhuru alisema.

Habari Nyingine: Uhuru azuru NGOME ya Raila na kuwaacha wenyeji na MACHOZI. Je, sababu ni nini?

Pakua APP mpya ya TUKO upate habari BURE!

Kalonzo Musyoka,aliyewahi kuwa naibu rais amekuwa katika serikali za awali kwa miongo mingi.

Raila aliyekuwa waziri mkuu baada ya ghasia za 2007 ameshikilia misururu ya nyadhifa katika enzi zake.

Changamoto kuu kwa Uhuru ni tatizo sugu la ufisadi linaloendelea kuathiri serikali.

Kisha kuna suala kuhusu kupanda kwa gharama ya maisha ambayo imesababisha bei za bidhaa za kimsingi kuongezeka kupita kiasi.

Habari Nyingine: Lupita Nyong'o anaishi na virusi vya HIV? Babake asema UKWELI

NASA katika kampeni zake imeahidi kushusha bei za bidhaa za vyakula nchini Kenya pamoja na kodi ya nyumba.

Katika mkutano huohuo, Uhuru alionekana kuwapuuzilia mbali wagombea binafsi.

Aliwahimiza wakazi kupigia kura wagombea wa Jubilee ili serikali iendelee kutekeleza miradi.

Habari Nyingine: Kiongozi wa Wiper atoa masharti makali kwa Raila

"Tupatieni wagombea wa Jubilee ili pamoja nao, tutaendelea kutekeleza miradi itakaoendelea kuboresha maisha yenu,” alisema Uhuru.

Awali TUKO.co.ke iliripoti kwamba Uhuru alikuwa amekaribisha uungwaji mkono wa wawaniaji huru waliounga mkono kuchaguliwa kwake tena.

Read ENGLISH VERSION

Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdiaYB2fZZmqZqho2LCqcHRrmSar5Ggsq6xwGatoqORobZuw8CnmKyhkaiubsPAZqWaq5FirrW7wGamppqZYrqircuupGajp5Z6uK3KnqWymV6dwa64