- Wabunge hao waliondoka baada ya gavana kukosa kuwapa fursa ya kuhutubia umma
- Walisema walikuwa na masuala nyeti waliyotaka yajadiliwe na rais
- Walimshutumu gavana Joyce Laboso kwa ubaguzi katika kutoa kandarasi kwa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Bomet
Kundi la wabunge kutoka kaunti ya Bomet waliondoka ghafla katika mkutano wa Rais Uhuru Kenyatta wakilalamika na kumshutumu gavana Joyce Laboso, dhidi ya kuwadunisha baada ya kuwanyima fursa ya kuhutubia umma.
Wakiongozwa na seneta wao Christopher Langat, na mwakilishi wa wanawake Joyce Korir, viongozi hao walisema walikuwa na masuala muhimu ya wakazi waliyotaka yashughulikiwe na rais.
Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka
Tukio hilo lilitendeka mnamo Jumatatu, Oktoba 22, baada ya Uhuru kuzuru Chuo Kikuu cha Bomet kwa ufunguzi rasmi wa Green Tuition Block katika taasisi hiyo.
Habari Nyingine: Aliyekuwa mkewe Pasta Kanyari asema ni mchoyo mno kuwashughulikia wanawe

Habari Nyingine: Mavazi ya walinzi wa pasta mrembo, Lucy Natasha, yawashangaza Wakenya
Wanasiasa wengine wanajumuisha seneta aliyeteuliwa Alice Milgo, wabunge Ronald Tanui (Bomet Central), Beatrice Kones (Bomet East), Brighton Yegon (Konoin), na Gideon Koskei (Chepalungu).
Wanasiasa hao wlaimshutumu gavana dhidi ya ubaguzi katika kutoa kandarasi za ujenzi wa chuo kikuu wakisema wafanyakazi wengi katika taasisi hiyo wanatoka jamii moja.
Habari Nyingine: Jacque Maribe amtaja Mike Sonko katika kesi ya mauaji ya Monica Kimani
Baada ya kuondoka katika mkutano, wanasiasa hao walihutubia vyombo vya habari huku rais akifungua rasmi kongamano la Lake Region Economic Bloc.
Habari Nyingine: Picha za Jacque Maribe na wanasiasa 6 mashuhuri Kenya, akiwamo Uhuru
Mojawapo wa masuala ambayo viongozi hao walitaka yashughulikiwe na rais ni kufurushwa katika msitu wa Mau na barabara duni katika kaunti hiyo.
Mnamo Jumapili, Oktoba 21, viongozi wa jamii ya Waluhya pia walilalamika baada ya viongozi wa eneo hilo kukosa kupatiwa fursa ya kuhutubia umma wakati wa sherehe za Mashujaa Day zilizoandaliwa Bukhungu Stadium kaunti ya Kakamega.
Read ENGLISH VERSION
Una taarifa motomoto au sakata ambayo ungependa tuichapishe? Wasiliana nasi kwa news@tuko.co.ke, mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdibYZ3hJFmrpqapaO0pnnWmmSbp52awW7DxKewnmWYlsCqvsBmrpqnnpm8rK2MpJitoZuWeqmtxaWYZrGRYsKpwdGuZKSvkWK4trzUrrGwmV6dwa64