Video ambayo ilitawala midomo ya wengi mwishoni mwa juma ni ile inayodaiwa kunaswa katika duka la kuuza nguo, Imenti House jijini Nairobi.
Makachero wa mtandaoni hata walitia bidii na kudai kufahamu ni duka nambari 32C kulipotokea sinema hiyo chafu.
Habari Nyingine : Mbwa wa babake Uhuru alikuwa na gari lake binafsi la aina ya Mercedes Benz - Lee Njiru

Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka
Zaidi ya kutambua duka, makachero hao walitafuta na kupata akunti ya Facebook ya mwenye duka hilo na hali hiyo ikamweka mmiliki huyo katika aibu kubwa na masimango.
Lakini ukweli kuhusu tukio hilo umebainika hatimaye, na ilivyo ni kuwa, video hiyo ilichangamsha sana mtandao na hata kufanyiwa kejeli aina mbalimbali ni porojo tu.
Habari Nyingine : Picha za polisi mwanamke akiongoza msafara wa magari kwa pikipiki zawafurahisha Wakenya
TUKO.co.ke imezama na kuibuka na ukweli, na ukweli huo ni kuwa, video hiyo ilipogolewa kutoka mtandao wa video za ngono, na wala si katika duka la nguo Imenti House ilivyokuwa imedaiwa awali.
Uchunguzi zaidi umebaini kuwa, ilinaswa katika duka la nguo huko Marekani na kusambazwa Aprili 2018.
Habari Nyingine : Wazazi wa marehemu Meru wasema alikuwa mwizi, wakataa kumpamba wakati wakimzika
Aliyeiweka video hiyo na kuigusisha hashitegi Imenti alikuwa akitaka kuwasilisha ujumbe wake kuhusu madai ya visa vya aiana hiyo kutokea katika maduka ya aina hiyo.
Read ENGLISH VERSION
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdiboFxgZVmrKSvlaG2brfUoaysrV2rtqWxzmawmmWdlrWirsBmoKeZqaSxorXWmmSkrZ6WwLitjKKknqaknnqpu9SsnGamkZ6%2FsK7IZ5%2BtpZw%3D