Gavana Kiraitu Adai Hakuna Mwanasiasa Atashinda Uchaguzi Kupitia Chama cha Jubilee 2022

August 2024 ยท 2 minute read

Gavana wa Meru Kiraitu Murungi amedai kwamba huenda chama cha Jubilee kikakosa kushinda viti muhimu katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2022.

Habari Nyingine: Mwanamke Afichua Jinsi Alivyotumia Mshahara Wake Kumlipia Mpenzi Wake Karo ya Shule

Habari Nyingine: Mbunge Rigathi Gachagua Adai Alitumia Mamilioni ya Pesa Kumpigia Kampeni Uhuru

Kiraitu amesema haya siku chache baada ya chama hicho tawala kutangaza mipango ya kuwatimua chamani wanachama waasi.

Akizungumza akiwa katika hafla ya uzinduzi wa matangi ya maji Agosti 3, Murungj alisema kwamba wanasiasa wakakamavu wanaotaka kugombea viti katika chama hicho huenda waka ambulia patupu.

Pia soma

Mbunge Rigathi Gachagua Adai Alitumia Mamilioni ya Pesa Kufadhili Kampeni za Uhuru

"Kitakua chama hafifu sana mwaka ujao na iwapo kuna mwanasiasa ambaye anataka kupoteza kiti chako basi asimame kwa tiketi ya chama cha Jubilee."  Alisema gavana huyo.

Aidha, chama cha Jubilee kinajivunia kuliongoza taifa baada ya kutwaa ushindi mwaka wa 2013 na 2017 mtawalia, huku rais Kenyatta na naibu wake William Ruto wakikiongoza chama hicho.

Habari Nyingine: Mwanawe Muammar Gaddafi Aliyedhaniwa Kufariki Dunia "Afufuka" na Kutangaza Anataka Urais Libya

Wachanganuzi wa siasa wanasema kwamba masaibu ya chama cha Jubilee yanatokana na kupoteza chaguzi ndogo katika ngome za rais Kenyatta hivi maajuzi.

Kudidimia kwa umaarufu wa chama cha Jubilee kumepelekea vigogo wa chama hicho tawala kuhamia vyama tofauti kikiwemo UDA ambacho kimehusishwa pakubwa na naibu wa rais William Ruto.

Madai hayo ya Kiraitu wameungwa mkono na wakili tajika Ahmednasir Abdilahi, aliyesema kwamba chama cha Jubilee kimekufa na kinastahili kuzikwa.

"Nafkiri Jubilee kitatokomea kama vyama vingine tu, huenda kikawa na waakilishi bunge wachache na waakilishi wa wanawake wachache" Alisema Ahmednasir .

Pia soma

Silas Jakakimba Adai Jalang'o 'Hajatosha Mboga' Kuwa Mbunge wa Lang'ata

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdkZ35yfZRmnpqukaOubrfIq5iirKVirqWtyGafmqOlo65uudaapZqrmZbAonnArZisoJmjsaJ51Jyfmp%2Blr7Zut9SpoK2hkWKwqa3MmmScoJFit7auyKWcnmViZX9zesetpKU%3D